Katika mchezo uliosukumwa ndani ya dimba la Amani hapa visiwani Zanzibar majira ya
saa kumi za jioni, Mtende wamekubali kichapo cha mabao 2-1 walipofungwa na
KMKM.
Mabao ya
KMKM yamefungwa na Mudrik Muhib katika dakika ya 26, pamoja na Faki Mwalim
mnamo dakika ya 45, huku bao la kufutia machozi la Mtende limewekwa kimyani na
mchezaji Abbas Nassib katika dakika ya 32.
Katika
mtanange huo mlinda mlango wa Mtende Yussuf Salum ametolewa uwanjani baada
ya kuoneshwa kadi nyekundu na mwamuzi
Rashid Farghan mnamo dakika ya 11
kutokana na kumzuia mchezaji wa KMKM Faki Mwalim pale alipokuwa katika harakati
za kutaka kufunga bao, na Mtende wakacheza watu kumi katika mchezo huo.
Kocha
msaidizi wa timu ya Mtende Kheir Ali Salum amesema kuwa bado wamekuwa
wakilalamika juu ya waamuzi wa mchezo wa mpira wa miguu Zanzibar,
“kitu
kinachosababisha matokeo ya timu yetu kuwa mabovu na kutokana na waamuzi wa
mchezo wa mpira wa miguu kwa sababu mpira wa miguu unaendeshwa juu yakanuni na
sheria kumi na saba na kanuni zake lakini utakuta uwanjani vitu kama hivyo
havitumiki.” Alisema kocha Kheir.
Kwa upande wake kocha Mkuu wa KMKM Ali
Bushir Mahmoud, amesema licha ya kuwa wamepata ushindi lakini vijana wake
hawakuweza kucheza kama vile alivyotarajia
“haidhuru
tumepata ushindi lakini vijana wangu hawakuwewza kupaform vile nilivotarajia,
niweze kusema hawakucheza vizuri hata kidogo kwa mujibu wa maelekezo ambayo
nimewapatiza, wanaonekana wanababaika uwanjani hawatulii na mpira wanasahau
kila kitu, hii inapelekea kuhatarisha
usalama wa mechi zijazo kwa sababu cheza vizur mechi moja hata kama
utapoteza lakini ucheze vizuri.” Alisema
kocha Bushiri.
KMKM sasa
wamefikisha alama (27) wakiwa nafasi ya nne (4), na Mtende wao wapo nafasi ya
kumi na tatu (13) na wana alama tisa (9).
No comments:
Post a Comment