Wednesday 23 March 2016

NASSOR KHALFAN: MAZOEZI NI KINGA YA MARADHI MENGI


KAMPENI "FICHUA VIPAJI"

Taarifa zinaonesha kuwa watanzania wengi wanasumbuliwa na maradhi mbalimbali katika miiliyao kama vile pressure, msongo wa mawazo, uzito mkubwa na mengineyo.

Hali hiyo imedaiwa kua inasaidiwa na mtu kutofanya mazoezi kwani mazoezi ni moja kati ya kinga ya maradhi mengi na yanapelekea mtu kuwa sawa kiafya.

Hayo yamebainishwa na mmoja miongoni mwa wachezaji wa mchezo wa ngumi aina ya Karati (shaurin) nchini Tanzania kutokea Kigogo  Mburahati   Uwanja  wa   Kifa   Balasa  Nassor Khalfan alipokua akizungumza na SALMA SPORT’S MEDIA katika mwendelezo wa kampeni ya “FICHUA VIPAJI” inayowatafuta wanamichezo mbalimbali kwa lengo kuwaonesha kwa wadau na kuwainua ili kufikia malengo yao kwa haraka kama walivyojipangia.

Khalfan ni mchezaji mahiri wa mchezo huo na mengi tuliongea yanayahusu moja kwa moja katika ngazi za michezo na maongezi yetu yalikua kama yafuatavyo.

Salma: wewe ndio umeshajiingiza huku katika michezo alau unamatumaini na malengo unawambia nini vijana wenzako?

Khalfan: siku nyingi  huwa nawaambia  vijana wenzangu ,jamani tusikae tu  nyumbani kufuga miili tunajenga maradhi  tufanye  sana   mazoezi   kwa   ajili  ya   afya    zetu .   kweli   watu  nawaambia   sana   na  matunda  yake  yataonekana tu.

Salma: Tanzania kunaonekana kuna michezo mingi lakini ipo chini tofauti na  nchi za wenzetu zinavyosifika ni upi ushauri wako ili kukuza michezo nchini kwetu?

Khalfan: ushauri  wangu   tunaiomba   serekali    itutengenezee     sehemu   maalumu  ya  kufanyia   michezo    na  hasa   sisi   watu   wa   karate, naamini tukipata sehemu nzuri za kuchezea nchi yetu itasifika tu maana tunaweza.

Salma: una malengo gani katika mchezo wako huu  katika siku za usoni?

Khalfan: malengo  yangu   ni    kufika   mbali  zaidi  katika   mchezo   huu,   baadae  niweze   kuipeperusha   bendera   yangu   ya   Tanzania   katika   mashindano  mbalimbali   ndani  nje  ya   tanzania.


Amemalizia kwa kutoa ushauri kwa serikali kuandaa mbinu maalum kwaajili ya kuinua viwango wa wanamichezo nchini ili kukuza sekta hiyo huku akizidi kutilia mkazo kufanya mazoezi kwani kufanya hivyo kutamkinga mtu na mashambulio ya maradhi mbalimbali yanayomnyemelea.

No comments: