Thursday 10 March 2016

WACHEZAJI 12 WA KVZ WAPANDISHWA CHEO, NDIO MANA WANA ARI ZAID NA KUFIKA HADI NAFASI YA 2 KWENYE MSIMAMO WA LIGI KUU



Siri imefichuka kwa upande wa timu ya KVZ ambayo inashiriki ligi kuu soka Zanzibar kanda ya Unguja ambapo Mtandao huu ulitaka kujua ni sababu ipi ilopelekea timu hiyo kuwa na kasi zaidi kwenye mzunguko huu wa lala salama ambapo wametoka nafasi ya 12 kwenye mzunguko wa kwanza na sasa wapo nafasi ya 2 kwenye msimamo wakiwa na alama 29.

Muandishi wa habari hii amemtafuta Khamis Abdul-hamid Hamid ambae ni katibu mkuu wa timu hiyo na kutaka kujua nini siri ya mafanikio yao.

Katibu huyo alisema ujio wa kocha Gwiji katika timu yao Abdul ghani Msoma na kupewa vyeo wachezaji wao 12 waliopandisha daraja timu hiyo ndizo sababu mbili kuu zilizopeleka mafanikio na mabadiliko makubwa klabuni kwao.

“ Kwa kweli siri ya mafanikio yetu ni ujio wa kocha Msoma na pia jeshi la KVZ limewapa nyota 2 wachezaji 12 waliopandisha timu msimu uliopita, ndo maana unawaona wachezaji wana ari sana sasa”. Alisema Khamis.

Wachezaji 12 wa KVZ walioengezwa cheo kutoka private mpaka kuwa COPROL ni Salum Songoro, Ali Mustafa, Suleiman Abdi (Sele Tz), Suleiman Ali, Rashid Maulid na Khatib Khamis.


Wengine ni Abdallah Suleiman, Abas Abdallah, Nassir Bakar, Makame Ali, Yakoub Bakar na Mussa Bakar (Edi Enzi).

No comments: