Rashford mwenye umri wa
miaka 18, amefunga mabao saba katika
mechi 13 tangu aanze kuchezea timu kubwa Februari.
Hodgson amependezwa
sana naye lakini amesema itakiwa vigumu sana kwake kumuweka kwenye kikosi cha
Ufaransa.
“Nafikiri utakuwa
uamuzi jasiri sana kumuingiza kikosini,” ameongeza Hodgson.
Rashford, amesalia na
miezi sita atimize umri wa miaka 19.
Alichezea timu kubwa ya
Manchester dhidi ya FC Midtjylland katika Europa League na akawafungia mabao
mawili.
Hodgson ana
washambuliaji wengi wakiwemo Wayne Rooney (Manchester United), Harry Kane
(Tottenham), Jamie Vardy (Leicester City), Daniel Sturridge (Liverpool) na
Danny Welbeck (Arsenal), Andy Carroll wa West Ham.
"Inaonekana kwamba
itakuwa vigumu (kumchukua) lakini ukizingatia wachezaji anaoshindana nao,
itakuwa vigumu kiasi,” amesema Hodgson.
No comments:
Post a Comment