Michuano ya Vijana chini ya umri wa miaka 20 Wilaya ya Chake
Chake imerindima jana na leo katika uwanja wa Gombani ikiwa ni hatua ya Nane
Bora.
Jana Jumamosi kulikuwa na michezo miwili, saa mbili asubuhi ikiwa
ni kati ya Ajax na Small Younng Islanders na saa 4 kukifanyika mchezo baina ya
Real Mkoroshoni na Stone City.
Katika mchezo wa asubuhi timu ya Ajax imefanikiwa kuibuka
washindi kwa magoli 2-1.
S/Y/Islanders ndio waliokuwa wa kwanza kujipatia bao
lilifungwa na mchezaji wake Khalfan Said katika dakika ya 12.
Bao hilo lilisawazishwa na Ajax kwenye dakika ya 21 kupitia
mchezaji wake Abuubakar Habibu huku la pili likiwekwa nyavuni na Said Mbarak Mkude
katika dakika ya 44.
Katika mchezo uliochezwa saa 4 asubuhi wa mashindano hayo
Real Mkoroshoni wakafakiwa kuondoka na ushindi kama huo wa mabao 2-1.
Goli la Stone City likifungwa na Said Khalfan kwenye dakika
ya 28 huku yale ya Real Mkoroshoni yakiwekwa wavuni na Jamal Amir dakika ya 51
na Shakir Aboud Said dakika ya 87.
Michezo ya leo ilikuwa ni kati ya Korea Star Soka na Madungu
City saa 2 asubuhi na saa 4 kulikuwa na mchezo kati ya Future Boys na Mabaoni
City.
Mchezo wa asubuhi timu za Korea Star Soccer na Madungu City
ziliumaliza mchezo huo kukiwa hakuna mbabe kwa kutoka suluhu 0-0.
Ama kwaa mchezo wa saa 4 asubuhi timu ya mabaoni City
wameibuka washindiki kwa kuichapa Future Boys kwa bao 1-0.
Ligi hiyo itaendelea tena Jumamosi na Jumapili kwenye uwanja
wa Gombani.
No comments:
Post a Comment