Monday 4 April 2016

YANGA YARUDI TENE KWENYE MZIMU WAO WAKIJIANDAA NA AL-AHLY.


Timu ya Yanga ya Dar-es Salam ambao ni wawakilishi wa Tanzania katika michuano ya Klabu bingwa Afrika imewasili visiwani Pemba leo kuweka kambi ya kujiandaa na mchezo wao dhidi ya Mabingwa wa soka wa Misri National Al-Ahly utakaochezwa Jumamosi.

Kikosi cha Yanga kikiwa na wachezaji 24 kimewasili kwenye uwanja wa ndege wa Pemba Airport majira ya saa 10 za jioni kwa ndege tatu tofauti za kampuni ya Al-Salaam Air na moja kwa moja kuelekea katika Hoteli ya Pemba Misali Sunset iliyopo nje kidogo ya mji wa Chake Chake.

Timu hiyo itaanza kufanya mazoezi kesho asubuhi katika uwanja wa Gombani hadi hapo Ijumaa itakaporudi Dar-es salaam kwa mchezo huo.

Yanga imefudhu katika hatua hiyo baada ya kuwatupa nchi timu ya APR ya Randwa kwa kuilaza mabao 2-1 huko Kigali na mchezo wao waliorudiana walitoka sare ya kufungana kwa bao 1-1 hivyo Yanga kufanikiwa kuvuka kwa jumla ya alama 4.


Mwaka uliopita Yanga ilitolewa katika hatua kama hii na timu ya National Al-Ahly kwa changamoto ya mikwaju ya penalt, baada ya Yanga kushinda nyumbani kwa goli 1-0 na wao kufungwa kwa 1-0 walipokwenda Cairo katika mchezo wa marudiano.

No comments: