Thursday 24 March 2016

BASKETBALL INAWEZA KUIPASIFA ZANZIBAR



Licha ya kusimama kwa mashindano ya mpira wa Basketball nchini Zanzibar lakini  timu hizo bado zinaonekana kutovunjika moyo kuendelea kuafanya mazoezi katika viwanja vyake.

SALMA SPORT’S MEDIA katika harakati zake iliwaona wachezaji wa timu ya New West katika uwanja wa Basketball wa MnaziMmoja mjini Unguja wakiwa wanafanya mazoezi uwanjani hapo.

Katika harakati hizo SALMA SPORT’S MEDIA ilibahatika kuzungumza na kocha wa timu hiyo Nassor Salum ili kutaka kujua ni kwa nini wanafanya mazoezi bila ya kuwepo kwa mashindano yoyote yale kwa sasa na wachezaji wanaichukuliaje hali hiyo?

Kocha Nassor  alisema kuwa wanafanya mazoezi hayo kutokana na system za chama huwa zinafanya  ligi za kushtukiza hivyo inawalazimu kufanya mazoezi kila mara ili yanapotokea mashindano basi iwe moja kwamoja kushiriki tu bila ya wasiwasi wowote.

“Tunafanya mazoezi kwa sababu ya kujiandaa sisi kama timu, huwa tunauzoefu na system ya chama cha Basketball Zanzibar kwa maana kwamba mara nyingi huwa kinatushtukiza tu ligi zao hazina muda maalum, hivyo sisi kama New West ni lazima tuwe tunafanya mazoezi binafsi ili hata ikitokea ligi basi tuwe vizuri”. Alisema kocha Nassor.

Aidha amesema kuwa timu kama timu wanaathirika kutokana na kutokuwepo kwa ligi yoyote.

“Tunaathirika kwa sababu timu kama timu inapokuwa inafanya mazoezi kwa muda mrefu wachezaji wanafikia hatua wanachoka, kwa hiyo mtu anapochoka na hapa hatulipani mwisho mtu anaona abakie nyumbani  au afanye shughuli zake nyengine kwa sababu  anafanya mazoezi muda mrefu lakini ligi hakuna”. alisema Nassor

Hivyo ametoa wito kwa Wizara husika  na kusema kuwa iache kutazama mchezo mmoja tu kwani michezo ipo mingi nchini na yote inanafasi nzuri ya kuitambulisha nchi,hivyo iitazame kama wanavyotazama sasa mchezo mmoja wa mpira wa miguu.

“Wizara iache kujiwekeza katika mchezo mmoja tu na waangalie na michezo mengine, kwa mfano football toka tunafumbua macho sisi, football wameing’ang’ania lakini michezo mengine hawakuipa nafasi kiasi ya kwamba hata football nao hawana wafikapo, lakini wangejaribu siku moja ama miaka fulani kuangalia hii michezo mengine huenda wakatoa wachezaji wazuri, huenda tukawa tuna ligi nzuri na pia huenda watu wakatengeza masoko ya uuzaji kwa sababu Zanzibar Basketball wanaipenda na hiyo football watu wanaipenda lakini kuna michezo mingi kama Netball, Vollball inakufa kwa sababu haina mashindikizo ya Serikali”.

Sambamba na hayo pia ameitaka kamati ya Basketball wawe wabunifu zaidi katika mchezo huo.


“Kamati ya Basketball kama  ipo na inanisikia wawe wabunifu kwa sababu bila ya wao hakuna kitu ambacho kitafanyika ni lazima wajikubalishe wakae na vilabu wapange”.alimalizia kusema kocha Nassor.

No comments: