Thursday 10 March 2016

TUNAKOSEA WAPI WAZANZIBAR, UKWELI KUHUSU SOKA LETU.


KAMPENI “FICHUA VIPAJI"

Masikio na macho wa wazanzibar yanatamani  kusikia na kuona siku moja Zanzibar ikitajwa kitaifa na kimataifa kukua kisoka kama zilivyonchi nyengine ambazo leo hii zikitajwa tu, kitu cha mwanzo watu watasifu kwa kiwango chao cha soka ni kama Brazil, Ujerumani, Uingereza na kwengineko.

Wengi sana wanajiuliza, ni kwanini wao waweze sisi tusiwese? Maswali haya ni mengi kwa mashabiki wa soka nchini mwetu lakini kwa ujumla hakuna alieambulia jibu zuri la suala hilo kila mmoja abakia na jibu lake likiwa ndilo au silo sawa tu.

Kwakua mimi mwenyewe ni mdau wa soka nambari one niliamua moja kwa moja niingie katika mchakato wa kutazama ni kwanini hasa wazanzibar leo hii tumekua nyuma katika soka ingawa ni nchi ndogo kigeographia na hata kiuchumi, lakini waswahili wanamsemo wao mashuhuri kabisa “mtu hujikuna ajipatapo” viwanja hivyohivyo tulivyonavyo mbona vinachezeka tu na kua na mafanikio,kwanini kwetu mafanikio ni kama Ngamia kupenya katika tundu ya Sindano?

Baada ya kuingia ndani kabisa kutazama nini chanzo hasa siku zote tuwe mkiani katika mashindano mengi ya soka , kitu cha kwanza kabisa tuligundua ni “SIASA’ ndio iliyotuharibia wazanzibar! asilimia sabiini (70%) ya wazanzibar maisha yao ni siasa tena imepenya katika kila kona ya michezo hapa nchini.

Tafiti hii ndogo  imegundua kua, hata viongozi wa soka katika mamlaka husika wanaongozwa na siasa kiasi ambacho hata maamuzi yao pia hutoka kisiasa saisa ya kugawanyika kwa mapande, hivi hapa kweli pana maendeleo katika jamii kama hii ya uongozi?

Mbona kwa wenzetu pia siasa ipo lakini haikua kama tulivyosisi, mfano mzuri hapo Kenya tu wala sio mbali nasisi, wanasiasa kama sisi, ni waafrika kama sisi, hata uchumi wao hatujapishana kiasi hicho lakini mara nyingi wamekuwa wakitupiga bao kila siku tuchezapo nao hapa sitaki nielezee sana mana mifano ipo mingi na wa mwisho juzi tu katika Kombe la Mapinduzi Cup kwa macho mawili imeshuhudiwa Kenya ikiondoka na kikombe wazanzibar wenyewe tukiwa tumetumbua macho tu tena tukisherehekea ushindi wa wenzetu,si vibaya kufurahia mafanikio ya mwenzako lakini ni aibu iliyoje kwa wenyeweji tena kombe lenyewe la mapinduzi yaliyoleta usawa kwa waafrika wa kizanzibar kushindwa nyumbani kwao.

Niliamua kutafuta wadau wa soka kuona jee kuna uhalisia wowote juu ya tafiti hii,wamwanzo kabisa niliekutana nae alikua alikua ni mchezaji wa Polisi  Mara daraja la kwanza Danny Manyenye.

Alisema wadau wa soka nchini wanatakiwa kupunguza au kuondosha kabisa “SIASA” katika medani za soka ili kuruhusu vipaji vya wachezaji kukua “viongozi wa soka nchini wamekua washabikiaji wa siasa mpaka huiingiza katika soka hivyo hupelekea kukinzana baadhi ya mitazamo  baadae hutofautiana wao kwa wao hatime kutokua na maendeleo katika timu husika.”

Aidha alisema kuwa nchi  ina vipaji vingi sana mitaani lakini wanaotakiwa kuviendeleza hawaonekani na badala yake  wanasubiri kumuona mchezaji anatoka chini mwenyewe kwa nguvu zake na anaposhindwa kutoka ndio humalizika kabisa kisoka lakini kama viongozi wanakua makini na ukuzaji wa vipaji vingezalishwa vingi tu sio kama sasa nchi inakosa dira kisa siasa.

Mwengine ambae hakupenda jina lake liandikwe amekubalina moja kwa moja na hoja kua siasa ndio sababu kuu inayopelekea soka letu wazanzibar kuwa chini, amesema ingawa zipo sababu nyengine nyingi lakini ni ndogondogo kubwa zaidi ni siasa.

“hata mgogoro wa sasa unaousikia ZFA huwenda ikawa kuna kitu katikati ambcho ni siasa,kwa kweli wazanzibari sisi tumuombe mungu sana  lakini sijui tunakwenda wapi”alisema

Wazanzibar siku zote wanatamani kusikia wapo juu kisoka ukweli vipaji vipo tele mitaani lakini kama siasa isipotazamwa kwa makini zaidi wazanzibar tutaishia hapahapa kukaribisha watu na kusindikiza wat utu.





No comments: