Saturday, 7 May 2016

KMKM YATOA KICHAPO CHA MABAO 4-2, LIGI KUU YA ZANZIBAR.

Timu ya Kikosi Maalum cha Kuzuia Magendo KMKM, imetoa kichapo cha mabao 4-2 walipocheza na Miembeni, katika mchezo wa ligi kuu ya Zanzibar kanda ya Unguja uliosukumwa ndani ya dimba la Amaan mjini Unguja.


Katika mtanange huo Miembeni walianza kupata bao la kuongoza lililofungwa na Ramadhan Hamza Kidilu katika dakika ya saba 7, Kidilu akarudi tena nyavuni mnamo dakika ya 16 kwa kuipatia Miembeni bao la pili.

KMKM walianza kupachika bao la kwanza kupitia mchezaji Haji Simba katika dakika ya 20, na dakika ya 34 Makame Haji Mngwali akaipatia KMKM bao la kusawazisha.

Timu hizo hadi zinakwenda mapumziko, zilikuwa sare ya mabao 2-2.

Kuanza kipindi cha pili tu katika sekunde ya 10, Faki Mwalim akapachika bao la tatu, na dakika ya 50 Faki Mwalim akarudi tena kwa kumaliza karamu hiyo ya mabao, na mchezo huo ukamalizika kwa KMKM kuibuka na ushindi mnene wa mabao 4-2 dhidi ya Miembeni.

KKMKM sasa wanashika nafasi ya pili wakiwa na alama 33, Miembeni wapo nafasi ya sita 6 na alama 30.

No comments: