Wednesday 9 March 2016

CHANGAMOTO NYINGI KATIKA SOKA LA TZ ZINARUDISHA NYUMA JUHUDI ZA WACHEZAJI.



"KAMPENI YA FICHUA VIPAJI"

Imesemwa kua soka la Tanzania ni lenye kukabiliwa na changamoto nyingi ambazo kwa namna moja ama nyengineyo hurudisha nyuma malengo ya wachezaji wa timu nyingi nchini hasa timu ndogondogo.

Kauli hiyo imetolewa leo hii na kocha wa timu ya   Vijana Renjers  wakati Tonge Nyama Dos Santos alipokua akizunguza na SALMA SPORT’S MEDIA leo hii katika kampeni ya “FICHUA VIPAJI” ikiwa ni mchakato wa kuwatembelea, kuwakagua na kuwaonesha hadharani wachezaji wadogowadogo wenye malengo makubwa na mazuri katika soka.

Amsema wachezaji wamekua wakifanya vizuri sana lakini changamoto nyingi  ndio tatizo.

Akielezea miongoni mwa changamoto hizo ni kama  timu kutokua na vifaa vya mazoezi  vya kutosha hali inayowafanya wachezaji kucheza katika mazingira magumu.

Pia maesema hata miundombinu ya viwanja wanavyochezea ni mibovu hivyo wachezaji hao hucheza tu haliya kua ni tofauti na mchezaji anavyotakiwa kucheza.

Amemtolea mfano mchezaji KANIY FUNDI wa timu yake akisema, ni mchezaji mwenye malengo ya juu katika soka, siku moja anatamani awe mchezaji mwenye kusifika nchini , mchezaji huyu ni fundi wa soka na hata wamashabiki wengi wanajikuta kumpenda kutokana na kiwangoi chake lakini bado pia yupo katika mazingira hayo.

Amesema KANIY ni mchezaji mwenye umri wa miaka 20 na anacheza nambari 9 katika timu hiyo ya Vijana Renjers ana dribo vizuri mpira  anapungunguza presha ya mashambulizi pia anajua kufunga kitaalmu zaidi.

Tonge Nyama Dos Santos ametoa wito kwa wadau wa soka nchini kuweka mazingira bora ya soka ili wachezaji wacheze katika mazingira mazuri ili vipaji viibuke.

No comments: