Sunday 28 February 2016

MAPAMBANO MPAKA KIELEWEKE



“Ingawa changomoto ni nyingi sana lakini nipambana kwa hali na mali mpaka kuona nafanikiwa katika kuyafikia malengo niliyojipangia katika maisha yangu ya  soka.”

Hayo ni maneno ya mchezaji wa timu ya Villa United FC ya visiwani Zanzibar  inayo wania nafasi ya kuingia 8 bora Juma Yusuf (James) wakati alipokua akizungumza na SALMA SPORT’S MEDIA leo hii  juu malengo ya kuwatazama wachezaji wenye nia ya kufika mbali  katika soka.

Mchezaji huyo amekua tegemezi kubwa katika timu yake hiyo kutokana na juhudi za makusudi anazozifanya katika kukuza soka la nchi nayeye mwenyewe.

James amesema mwenye umri wa miaka kumi na saba (17) ameamua kufanya jitihada kubwa ya mazoezi na kuiga kwa wachezaji wa kimataifa namna ya uchezaji wao ili nae siku moja acheze soka nje ya nchi kwa lengo la kuliletea sifa taifa lake kama ilivyo kwa mataifa mengine.

Amesema katika kuyafikia malengo yake hayo amekua akikabiliana na changamoto nyingi sana ambazo kwa namna moja ama nyengineyo kama mtu hatokua makini zinaweza kumrudisha nyuma na kufeli.


Amezitaja changamoto hizo ni pamoja kujiunga kwenye timu ukawa unafanya vizuri lakini kwa uzuri wako hatimae ukaanza kusemwa ukaambiwa hufai na kukukata tamaa kwa makusudi wakati sio uhalisia ulivyo kumbe ni roho mbaya tu zilizojengeka kwa baadhi wa wadau na viongozi.

Akijibu suala la mwandishi wa habari SALMA HASSAN kua analizungumziaje suala la vipaji kutojaliwa na kuthaminiwa amesema  vipaji nchini mwetu vimo tena vingi sana lakini tatizo liliopo ni kua havizingatiwi wala havithaminiwi na badala yake  vinaachwa vikifa  vijijini.

Sambamba na hayo James ametoa wito kwa wadau wa soka na wahisani kwa ujumla kuwawezesha wachezaji wadogo wadogo kwani wanauwezo wa kutosha katika soka lakini wanashindwa kuonekana kutokana na kutowezeshwa.



Pia amemalizia kutoa ushauri kwa wachezaji wenzake ambao wanamalengo kama yake kujituma katika mazoezi na kutovunjika moyo kirahisi pia kuwasikiliza walimu wao vipi wanavyowaelekeza na kutumia mafunzo hayo kama inavyotakiwa.

No comments: