Tuesday 15 March 2016

KIVULUGE AFICHUA SIRI YA MAFANIKIO YA SOKA TANZANIA.

 


Mchezaji nambari sita (6) wa timu ya Mbeya City team “B” Ligi kuu Tanzania bara Majdi Shabani  Kivuluge amesema soka la Tanzania linaonekana kukua kiasi fulani tena ni la kuvutia lakini bado linakabiliwa na changamoto nyingi ambazo kwa namna moja ama nyengine zinaweza kurudisha nyuma maendeleo hayo.
Kauli hiyo ameitoa leo hii alipokua akizungumza na SALMA SPORTS MEDIA juu ya muonekano wa soka la Tanzania ukilinganisha na mataifa mengine.
Kivuluge amesema soka la Tanzania linakua sana na hii inasababishwa na timu kua na ushindani mkubwa sana hivyo kila mmoja inampasa kuonesha ari ya kushinda na ndio maana ikaonekana kukua kwa kiasi Fulani.
“soka limekua kwa kiasi kikubwa sana mana kwasasa Ligi inaushindani mkubwa sana tofauti na zamani, leo kila timu ina mashabiki wengi na kila mmoja anajihisi yeye ni mshindi na hakuna anaekubali kushindwa”alisema Kivuluge.
Akizungumzia upande wa changamoto zinazolikabili soka nchini ambazo ndizo zinazodhoofisha ukuaji wake mpaka kufikia pale panapo takikana amesema katika timu nyingi viwanja wanavyochezea ni vibovu havisatahili kabisa kwa hadhi ya soka.
Pia amesema kuna uzorotaji na uhaba wa wadhamini wa kudhamini michuano mbalimbali, amesema bila ya kuwepo wadhamini hakutokua na soka imara ni lazima wajitokeze kusapoti nchi yetu.
“ hebu tazama viwanja ni vibovu  na ligi hazina  wadhamini wa kutosha,  sanasana  unakuta team muda mwingine inaishiwa pesa ya kuwalipa wachezaji unakuta miezi mitatu mchezaji hajalipwa unafikiri patachezeka mpira apo”alisema Kivuluge.
Kivuluge amesema ili kuinua zaidi soka nchini ni lazima wadhamini wajitokeze kwa wingi na serikali ijitahidi kuongeza bidi za kuwatafuta hapo soka ndipo litakapokua.
Aidha ametoa wito kwa upande mwengine wa kukuza soka kuwa, ni muhimu sana kuwa na mpango wa kukuza na kuwaendeleza vijana kwani wapo wengi mitaani na wanavipaji lakini hakuna anaewajali “Viongozi waweke mpango endelevu wa kukuza vijana kuwe na academic nyingi na kila team Iwe na uwanja wake kama unavyona kwa Azam fc”. Alisema Kivuluge.

No comments: