Tuesday 15 March 2016

BADO KUA KAMA WENGINE KUSIFIKA KWA SOKA.

Mchezo wa soka  nchini  Tanzania unaonekana kuwa  bado kukua upo chini  ukilinganisha na nchi za wenzetu zinazosifika kwa maendele ya mchezo huo.
Kauli hiyo imetolewa le na Goalkeepar  wa timu ya Makumba fc  ligi daraja la pili  ngazi ya mkoa Dar es salam Babuu Adinan (De gea) alipokua akizungumza na SALMA SPORT’S MEDIA  juu ya taswira halisi ya soka chini.
Katika mzungumzo juu ya taswira hiyo tulibahatika kuzungumza  mengi sana na maongezi yetu kwa uchache yalikua kama ifuatavyo.
Salma Hassan: unalizungumziaje soka la Tanzania  kwa ujumla kiukuaji wake?
Adinan : Soka letu  bado sana ukilinganisha na nchi nyengine za wenzetu sisi bado tupo nyuma na  hali hii  inatokana na viongozi wenye dhamana na soka.
Salma Hassan : kivipi viongozi  hawa  wanashindwa kuliendesha soka vizuri mpaka tukawa kama wenzetu ambao leo hii wamekua mfano mzuri duniani?
Adinan : Sababu kuu ni umimi na ubinafsi uliyotawala na si jambo jengine ingawa yapo lakini hili ni kubwa lao.
Salma Hassan: ok  sasa nini kifanyike ili soka letu likue nasi tuwe kama wengine wenyekutajika?
Adinan : kama  viongozi wataacha hiyo tabia ya umimi na ubinafi tu  soka la bongo litakuwa kwa sababu kuna vipaj vingi vya ukweli na wapenda soka wapo wengi tu.
Hayo yalikuwa ni mazungumzo kati ya mwandishi wetu wa SALMA SPORT’S MEDIA pamoja na mlinda mlango wa timu ya Makumba fc wakati tulipokutana nae na kuzungumzia kuhusu soka letu la Tanzania.
 

No comments: