Hakika hiki ni kipaji
cha kupigiwa mfano nchini mwetu, mafanikio ndio yake dira na malengo mema ndio
aliojipangia, mengi sana amekumbana nayo katika soka kama ni changamoto lakini
bado anaendelea kuzipembua na kuziweka upande mpaka pale apatakapo afike.
Amedai kua baadhi ya viongozi wa soka nchini huongozwa na
maslahi yao binafsi katika utekelezaji wa majukumu katika timu hivyo ikitokea
tu kocha huyu kama hakukupenda hata ufanye nini huwezi kuibuka kidedea kwake.
Bila ya shaka unahamu na shauku ya kumjua huyu ninani
tunayemzungumzia hapa, si mwengine isipokua ni mchezaji kipaji alieanzia timu ya
Spark Youth ya Mombasa nchini Kenya Raymond S Nkwande Mdudu.
Huyu ni mtanzania mwenye umri wa miaka 22, alisafiri sana
kisoka ndani na nje ya nchi na mengi sana alikumbana nayo katika safari yake
hii, kipaji chake ni chakupigiwa mfano laiti kama inatunzwa nuru hii ni lazima
ing’are vyema na kumurika nchini zokte katika medali ya soka.
Twende pamoja uone historia fupi kisoka ya mchezaji huyu
pamoja na majanga yaliomkuta kisha njoo
na jawabu katika suala hili, inakuaje kama atajaliwa na kuthaminiwa nchi yetu
itakua wapi kisoka?
Timu yake ya kwanza aliyowahi kuchezea ni Chipukizi ya Tabora mnamo mwaka wa 2009 baada
ya kuonekana kipaji chake ni kizuri kinakua kadiri ya siku zinavyokwenda basi
pia iliamuliwa kuondoshwa timu hiyo na kupandishwa juu kidogo timu ya kanda ya
magharib Umiseta katika mwaka 2010.
Hapo pia hali ilikua kama kawaida yake alipaform vizuri baadae kulipita mchujo wa kutafuta tano bora
katika timu hiyo hatimae alifuzu.
Kibaha Kipinguambae ni mdau na mwalimu mzuri wa soka alimuona
na akaamua kumpeleka katika skuli yake ya lord Baden Powell 2010 ili kumuendeleza
kisoka na kweli alikua.
Hakikaya uchezaji wake
akiwa kiwanjani hufurahisha wengi sana hasa kwa mipira anavyoinasa miguuni
mwake kanakwamba Kiwembe kutua katika Sukamu, mwaka 2012 akafanikiwa kuingia
Yanga youth kama ni maendeleo makubwa kwake, apo amefanya majaribio ya
kutazamwa na mwishowe alikubalika.
Kama kawaida ya mambo mengi duniani huwa na pande mbili ya
faida, hasara au changamoto hapa sasa kazi ndipo ilipoanza, madudu mengi
yalianza kuibuka, ubabaishaji ukaanza
kisa tu haikua chaguo la mtu fulani machoni mwake ikapelekea kuachwa katika
timu hiyo.
Baada ya miezi minne Mdudu hakurudi nyuma alijaribu tena bahati yake akiamini kipaji alichonacho anaweza kukiendelea na kufikia malengo yake ya kua mchezaji mzuri wa kuitangaza nchi yake ndani na njea, mashabiki wake walimtia moyo kua anaweza na kila kona ilithibitikia kweli kama naweza, alikwenda Azam Youth Team hapa nasema “asikwambiae mtu kulikua na watu zaid ya 250 lakini kwa jitihadi niliyoionesha tulibaki watano tu nami ni mmoja wao, fikiria wanne tu ndio walioruhusiwa kubakia camp kasoro mimi tu peke yangu sjui why” alisema Mdudu kwa huzuni ya kusikitisha akionesha ni namna gani baadhi ya viongozi hapa nchini wanavyoshiriki kwa makusudi kuua malengo ya wenziwao.
Baada ya miezi minne Mdudu hakurudi nyuma alijaribu tena bahati yake akiamini kipaji alichonacho anaweza kukiendelea na kufikia malengo yake ya kua mchezaji mzuri wa kuitangaza nchi yake ndani na njea, mashabiki wake walimtia moyo kua anaweza na kila kona ilithibitikia kweli kama naweza, alikwenda Azam Youth Team hapa nasema “asikwambiae mtu kulikua na watu zaid ya 250 lakini kwa jitihadi niliyoionesha tulibaki watano tu nami ni mmoja wao, fikiria wanne tu ndio walioruhusiwa kubakia camp kasoro mimi tu peke yangu sjui why” alisema Mdudu kwa huzuni ya kusikitisha akionesha ni namna gani baadhi ya viongozi hapa nchini wanavyoshiriki kwa makusudi kuua malengo ya wenziwao.
Anadelea kueleza “ kulikua na Coach Muhindi Vivec alikua
ananiamini sana, mimi striker2 mido2 bek1 sikuletwa na mtu, nlienda try mimi
mwenyewe, hata ukiwauliza Azam players leo hii basi wananijua kwa uwezo wangu, nlikua naitwa
Kavumbagu nilikua maarufu sana pale kuzidi hata niliowakuta, huyu Mrundi
kavumbagu alikua Yanga.
Mpaka leo hii Raymond S Nkwande Mdudu hajui nini kilicho
msibu hapo, ukizingatia kwanini anafaulu vizuri na anakubalika lakini baadae
huanza bifu, alichokigundua ni kuwa, kumbe ni ile kuwa juu zaidi kisoka kuliko
wenyeweji wa hapo ambao walimu ndio walikua matarajio yao kwa maslahi yao,
anasema “kuna baadhi ya viongozi naweza kukutajia wananiambia Coach kasema
nisije kumbe ni uwongo mtupu wa kutaka nibakie nyumbani tu ili nionekana
mkorofi baadae wapenyeze fitina zao, nikawa nakaa tu home, wachezaji wenzangu
wananiambia natafutwa na Coach nikienda anaulza mbona sikuoni siku hizi jibu
langu ni kua nimeambiwa nisije kidogo kuna mambo yanarekebishwa hata mwenyewe
anashangaa”alisema Mdudu.
Mpenzi msomaji wetu hii ndio Tanzania kisoka unajionea
mweyewe hali halisi ya mambo, haya ndio maisha ya kijana huyu katika maendeleo
yake ya soka na sasa yupo tu kipaji chake anakiendeleza mitaani lakini bado
hajakata matumaini washauri wa mambo walimwambia alikopita alipita sipo hakua
na mtu nyuma yake alikua yeye peke yake hata iweje hawezi kuonekana.
Akizungumzia kuhusu wachezaji wa vijijini Nkwande amesema vjijini kuna wachezaji wengi na wazuri sana wakiwezeshwa wanaweza,amesema
wanacheza Ndondo na wanafanya vizuri.
“wachezaji hawa wa vijijini
wapatiwe walimu, wapatiwe vifaa hasa mipira imekua tatizo kwao, viongoz
waende huko tena waanzie chini shule za msingi, wawape misingi ya soccer vijana
wakiwa wadogo”alisema Mdudu.
Amesema amekaa kenya muda mwingi lakini hakuona vipaji vya
hali ya juu vya soka kama nchini Tanzania “humu bwana kuna vipaji visi sana
lakini ndio ivyo”alisema Mdudu.
Mwisho kabisa amewashauri viongozi wa soccer waache
ubabaishaji na kuchagua wachezaji kwa kujuana hapo ndio soccer nchini
Tanzania litakua.
Pia viongozi na wadau wa soka watazame sana vipaji hasa
maeneo ya vijiji kwa sababu vipo vingi
lakini havipati nafasi ndio maana hakuna wachezaji wengi walio .
No comments:
Post a Comment