Wednesday 9 March 2016

SAMATTA WAMO WENGI TANZANIA

KAMPENI “FICHUA VIPAJI"


Ili kusifika na kua bora katika soka ni lazima kufanyike juhudi za makusudi kwa mchezaji mwenyewe kimazoezi huku akinuwiya lengo lake alilolipanga kulifikia hapo anaweza kuwa juu kama walivyowengine ambao leo hii tunawasifia kila pembe ya nchi.

Ushauri huo umetolewa  leo na mmoja kati ya Manager wa Stend United FC  ya ligi kuu Tanzaniabara Ramadhan Mohammed alipokua akizungumza na SALMA SPORT’S MEDIA katika “KAMPENI YA FICHUA VIPAJI” inayowatembelea na kuwakagua wachezaji wadogowadogo na hata kwa wachezaji au timu kubwa ili kutoa ushauri wa namna gani inavyowezekana mpaka wachezaji wa chini kuwa juu na hatimae kuliinua soka la Tz kwa ujumla.

Mohammed amesema wachezaji vipaji wapo wengi nchini lakini wanaoonekana ni wachache, amesema ni lazima kwa wachezaji wadogowadogo wazidishe bidii katika mazoezi siku moja watatajika tu.

“wachezaji vipaji wapo na wazidishe  juhudi tu mpira siku zote ni mazoezi  juhudi zao ndizo zitakazo wafanya watoke kimpira na kulitangaza vyema taifa, nafikir vijana wengi wameona mfano mzuri kutoka kwa Mbwana Samata,hivyo wazidishe  juhudi na kuzingatia kile wanachofundishwa ndio kitu kikubwa”alisema Mohammed.

Amesema ili kuinua vipaji vya wachezaji, timu kubwa kubwa zinatakiwa ziwe na Academy ili wawafunze vizuri vijana, amesema hata TFF hilo waliwahi kuliona lakini mpaka sasa hafamu utekelezaji wake “nakumbuka TFF waliweka mikakati endelevu kwa kila timu inayoshiriki ligi kuu kua na team “B” lakini hilo pia naona hasa kwa team ndogo zinashindwa kufanya hivyo kulingana na uwezo wao hasa kiuchumi kua mdogo” alisema Mohammed.

Sambamba na hayo amesema soka la Tz kwa ujumla linaonekana kukua kidogo tofauti na zamani kwa sababu timu nyingi sasa zinaonekana kuwa na upinzani wa hali ya juu ingawa changamoto zilizopo zinarudisha nyuma juhudi za wachezaji baadae kutokua kwa kiwango kinachoridhisha.

Mohammed ametaja changamoto kubwa inayozikumba timu nyingi nchini na kufanya hata soka kwa ujumla kuzorota ni uchumi mdogo waliokua nao wachezaji na timu zao.

Amesema Lazma team ziwe na vyanzo vya kupatia mapato pia kutafuta wafadhili na hata watu wanao miliki makampuni wajitoe pia katika  soka ili kuweza kusaidia mchezo wa mpira wa miguu  kukua zaidi na zaid.

Mwisho kabisa ametoa wito kwa Serikali kupitia mamlaka husika , ili kuendeleza na kukuza vipaji kwa vijana kurudishwe michezo mashuleni, kwenye makampuni yawepo mashindano mbalimbali kama UMISETA na pia zianzishwe Academy hata kama sio kila mkoa ,  kila kanda ipate Academy 2/3


Amesema TFF ikifanya  hivyo  anaamini mpira utaendelea kukua na kutapatikana  akina Samata wengi nchini Tanzania

No comments: