Tuesday 8 March 2016

SEMBE:KUANDALIWE KAMATI MAALUM ZA KUKUZA VIPAJI NCHI INAWEZA KUTAJIKA

"KAMPENI YA FICHUA VIPAJI"
Sembe ni alievaa flana nyekundu na kaptura nyeusi wakiwa na furaha baada ya kumaliza game ya kirafiki BWELEO.

Mmoja miongoni mwa Mawinga mahiri Zanzibar Sembe Aliy (25) amesema kuwa lengo lake hasa katika soka ni kuhakikisha siku moja anakua mchezaji maarufu na mashuhuri katika medani za soka nchini.

Ametoa kauli hiyo ya kusisimua wakati alipokua akizunguza na SALMA SPORT’S MEDIA leo hii katika kampeni ya “FICHUA VIPAJI” ikiwa ni mchakato wa kuwatembelea, kuwakagua na kuwaonesha hadharani wachezaji wadogowadogo wenye malengo makubwa na mazuri katika soka.
Sembe ni mchezaji wa kawaida katika timu za mitaani  “BWELEO” Zanziabar amesema siku zote amekua akijituma kwa mazoezi ya kila aina kuhakikisha siku moja anafikia lengo lake hilo.

Amesema vipaji vipo vingi Zanzibar lakini vinaishia mitaani hasa maeneo ya mashamba, hii inatokana na kutothaminiwa kwa wachezaji wadogowadogo hasa wa vijijini.

Sembe amesema serikali kupitia ZFA waandae kamati ya kukuza vipaji na kutoa sapota kwa wanasoka wa chini kwani kuna wachezaji wazuri ambao wakiibuliwa wanaweza kulitangaza taifa vizuri ndani na nje ya nchi.

Sembe ni mchezaji anaemudu vizuri kucheza nambari saba (7) na kumi na moja (11) mashabiki wengi wa BWELEO wanamkubali kwa kazi yake lakini mpaka leo hii amebakia mitaani.

SALMA SPORT’S MEDIA imeridhishwa na kiwango chake na iwapo hatua za kuwaenzi vijana hawa zitachukuliwa kwa hamasa zaidi tunaamini Semba atailetea sifa nchi kitaifa na kimataifa.

Ndoto zake ni kuwa Super star siku moja lakini mpaka sasa anaishia katika timu za “maskani” na ukimtazama kiukweli utavutiwa na uchezaji wake akiwapo uwanjani.

Akizungumzia changamoto anazokabiliana nazo katika soka amesema kitu cha kwanza kuzaraulika kwa wadau wa soka iwe ngazi zinazofanana au hata za juu yake.


Sembe amemalizia kwa kusema ataendelea na msimamo wakehuohuo katika mazoezi na kucheza soka kadiri iwezekanavyo mpaka atakapoyafikia malengo yake huku akiwaomba wadau wa soka nchini kutilia mkazo na nguvu katika kuwawezesha wachezaji wadogo kwa kuwasapoti na kuwakuza akiamini wanavipaji vya hali ya juu lakini vinashindwa kuoneakana.

No comments: