Sunday 3 April 2016

VIPAJI VYA KUTOSHA VIPO CHAAJABU TUPO CHINI


KAMPENI “FICHUA VIPAJI”

                     wambele mwenye mpira ni Braythoni Japheti 

Mlinzi wa timu ya Simba “B”upande wa kushoto  Braythoni Japheti ameamua kutoa mtazamo wake kwa soka la Tanzania huku akijiuliza kwanini linashindwa kukua wakati vipaji vipo vingi nchini.

Braythoni Japheti ameyasema hayo jana wakati alipokua akizungumza na SALMA SPORT’S MEDIA  juu ya uwoni wake kwa soka nchini Tanzania.
Amesema “Ukiangalia vipaji Tanzania vipo vyakutosha ila ukuzaji  wa vipaji  hivyo  ndio imekua tatizo”alisema Braythoni Japheti

Amesema ukitazama vipaji vya vijana waliopo mitaani utashangazwa kwanini nchi inashindwa kupiga hatua kubwa katika maendeleo ya soka, amesema kila kona watoto wacheza tena kwa viwango vizuri na vya kuridhisha lakini hawana matunzo na ndio maana huishia mitaani tu.

Aidha amesema ni hali ya kusikitisha kwa wachezaji wadogowadogo nishinda kupata usaidizi ili kukuza vipaji vyao “ Yani ukiwa na kipaji itabidi ufanye jitihada zako mwenyewe ndio upate kuonekana la si hivyo itaishia stori tu, sasa hapa ndio tunafanya nini”

Sambamba na hayo Japheti amesema  “ Vituo vya ukuzaji vipaji  nchini  bado havijawa vyakutosha kwasababu ukiangalia saivi ukiwa na kipaji bila kufika Dar  basi wewe kiwango chako kitaishia vilabu vya chini hutokuja kuonekana hata siku moja ”alisema  Japheti

Ametoa wito kwa viongozi  kwa kusema kua wanatakiwa wawe makini kwa kuliona hilo kwani vipaji vipo vya kila aina na nchini inaweza kupiga hatua kwa wachezaji hao .


Amesema kuweka vituo vingi vya ukuzaji vipaji  kila kona Ya T’z kutajenga hamasa na vijana watacheza kwa moyo zaidi baadae mafanikio yanajitokeza yenyewe.

No comments: