Sunday, 8 May 2016

BAYERN MUNICH YATAWAZWA RASMI BINGWA WA LIGI YA BUNDESLIGA

Bayern Munich players celebrate winning the Bundesliga for a record fourth successive season

Timu ya Bayern Munich yabeba taji la ligi ya Bundesliga kwa mara ya 4 mfululizo.

Bingwa wa taji la ligi kuu ya soka ya Bundesliga nchini Ujerumani alibainika hapo jana baada ya mechi za wiki ya 33 kuchezwa.


Mabingwa watetezi Bayern Munich waliweza kuhifadhi taji lao kwa mara ya 4 mfululizo baada ya ushindi wa 2-1 dhidi ya Ingolstadt kwenye mechi iliyochezwa hapo jana.


Bayern Munich ilitawazwa bingwa wa taji la Bundesliga kwa kuwa ilitakiwa kupata ushindi ikiwa imesalia wiki moja kabla ya ligi kumalizika.


Kwa mafanikio hayo, Bayern Munich imeweza kunyakuwa taji lake la 26 la Bundesliga na kuendeleza historia yake ya kuwa kilabu yenye mataji mengi zaidi Ujerumani.

No comments: