Saturday 27 February 2016

SOKA LA TZ NI LA CHANGAMOTO


Mchezo wa mpira wa miguu nchini Tanzania unaonekana kua na changamoto nyingi zinazopelekea kutokukua kwa viwango vya juu kwa timu mbalimbali hapa nchini.

Hayo yamesemwa na mmoja miongoni mwa dawau wa soka nchini Ahmad Ali Bakar kutoka Dar es Salam alipotoa maoni yake juu ya soka la Tz kwa mwanamichezo wako Salma Hassan.

Amesema hali hiyo inasababishwa na baadhi ya viongozi kutokua na umakini na kazi zao lakini pia baadhi ya timu kubwa kutojali na kuthamini vipaji vya wachezaji akisema kua wakikuona unafaa na kiwango chako kipo vizuri wanakuchukua ila ukichuja tu kidogo basi huna tena thamani katika timu hiyo amesema huko ni kupoteza vipaji.


Amemalizia kwa kutoa ushauri wake kwa viongozi wa soka nchini kuwa wafanye kazi za ufundishaji kwa umakini na kuweka upande maslahi yao binasi.

No comments: