Tuesday 15 March 2016

TOFAUTI YA ZENJ NA TANZANIA BARA NI MOJA TU KWA SOKA.

Wadau wa soka nchini wameonesha kukasirishwa na tabia ya baadhi ya wachezaji wengi kwa upande wa Zanzibar kwa tabia ya kucheza soka kama ni mazoea tu au burudani ya kawaida pasipo na kuutilia nguvu, hali ambayo imedaiwa kuwa ndio sababu moja wapo ya timu za Zanzibar kutofanya vizuri katika mashindano tofauti.
Mmoja miongoni mwa wadau wa michezo kutoka Tanzania bara Bw:Abdul Jimbo pia amelizungumzia soka la Zanzibar  na wachezaji wake kwamba bado wanachukulia mpira kama ni kitu cha kawaida wakati wenziwao wa Tanzania bara wanachukulia kama ni sehemu ya ajira na ndio maana hujituma kwa bidii na wanaonekana wapo juu zaidi ya visiwani.
“Zanzibar kuna vipaji vingi sana na kuna watu kama wataamua kweli basi soka litachezwa lakini tofauti ya Zanzibar  na Bara ni moja tu, wachezaji wengi wa Zenji  wanafanya mpira kama sehemu ya kupata burudani tu ila wenziwao wa Bara wachezaji wanafanya mpira kama ajira yao ndio maana utaona soka la Bara kwa upande Fulani hivi lipo juu tofauti na Zenji”alisema Jimbo.
Jimbo amesema ni lazima wachezaji wa Zanzibar sasa wabadilike na kutilia mkazo zaidi mchezo wa soka akisema duania ya sasa, soka ni ajira na inayolipa ikiwa utafanya kazi nzuri.
Kwa uapnde mwengine  ameshauri mamlaka za soka nchini kuzidisha vyuo vya mpira kua wingi na ufundishaji uwe wa kuwafanya watoto waone mpira ni kama sehemu ya maisha yao hivyo kutainua viwango vya soka na hatimae taifa litasifika kama yalivyomataifa mengine.
Ametolea mfano wa taifa la Brazili akisema  mpira ni moja ya utamaduni wao, hivyo mtoto tokea anakua anafahamu kama soka ni sehemu ya ajira.
Pia amesema walimu wa soka  wawafunze wachezaji wao jinsi ya kucheza mpira wa ushindani na sio mpira wa burudani tu.

 

 

No comments: