Kiungo
Mshambuliaji wa Kijichi Ali Jecha “Vigema” kesho anatarajiwa kurejea mazoezini
katika klabu yake ambapo alikaa majeruhi kwa kipindi kirefu.
Jecha
amewaahidi mashabiki wake wategemee makubwa kutoka kwake ambapo anataka
kuisaidia timu yake ya Kijichi kwenye ligi kuu soka ya Zanzibar kanda ya
Unguja.
“
Hali yangu ya afya sasaivi ipo vizuri na kesho naanza mazoezi katika timu yangu
ya Kijichi, wapenzi wangu na wa Kijichi wote waniunge mkono naamini ntakuwa
vizuri na ntawafurahisha”. Alisema Ali (Alcantara)
Kwasasa
Ali Vigema anakipiga timu ya Kijichi kwenye ligi kuu soka Zanzibar Kanda ya
Unguja na hakuwahi kucheza hata mchezo mmoja kwenye ligi hiyo kutokana na
kusumbuliwa na majeruhi.
Mchezaji
huyo anauwezo binafsi wa kumiliki mpira na kuudhibiti bila ya adui kumpokonya,
pia ana uwezo mkubwa kupiga chenga na kupiga mashuti makali langoni mwa
wapinzani.
Jecha
pia aliwahi kuchezea timu ya Kilimani city, Maji maji, Magomeni na alipokuwa
mdogo kwenye ligi za Central Wilaya ya Mjini alikipiga kwenye timu ya
Javerlion, Aston Villa, FC Ajax ya Bakari Rais, Leeds United ya Babu Khatib na
FC Natural na alikuwa anaogopewa sana na timu pinzani kutokana na uwezo wake
binafsi.
No comments:
Post a Comment