Tuesday 1 March 2016

MAKOCHA ZENJI JITOSHAUTISHENI NA WANASIASA.




Walimu wa soka nchini (makocha) wametakiwa kujitofautisha na wanasiasa na badala yake wafanye kazi za kiuwalimu ili kutoa vipaji vya uhakika nchini ili baadae kuliletea sifa taifa.

Wito huo umetolewa na mchezaji wa zamani wa mpira wa miguu wa timu ya “Magirisi” daraja la pili na mdau wa michezo leo hii Bwnana Maulid  Ali (MAJIN) wa Meli nne  Zanzibar  wakati alipokua akizungumza na mwanahabari  wako Salma Hassan juu ya maendeleo ya soka la Zenji.

Amesema soka la zenji linashindwa kukua kwa sababu baadhi ya walimu wamekua  hawana tofauti na wanasiasa kwa kile alichokiita porojo jingi.

Majin amesema walimu hao wamekua ni wakuropokwa ovyo kwa maneno mengi pasipona ufundishwaji mzuri hatime  timu zinadumaa na kila siku zinakua katika kiwango kile kile.

“soka la zenji  kwa sasa  ni tofauti sana zamani kwa sababu  viongozi wanaoongoza soka siku hizi sawasawa na wanasiasa hawana zaidi ya kuporoja kwingi”alisema Majin.

Akijibu suali la mwandishi wa habari hizi kwanini kumekua na tabia ya kununua wachezaji kutoka nje ya nchi wakati inasemwa kuwa nchini mwetu kuna vipaji lakini havithaminiwi amesema “Kwanza wachezaji wetu wa ndani hasa hapa zenji wanachukulia mpira ni kama starehe lakini kwa wenzetu mtu ni kama ajira yake, ninachotaka kuwambia waufanye huu mpira ni kama ajira,kwa hilo tu  nahakikisha tutafika mbali”


Pia amotoa wito kwa viongozi ambao hawana utashi wa mpira waache kushuhulikia kazi hiyo  kwasababu ni moja kati ya pingamizi za timu kutoshafanya vizuri na badala yake kuwe na  na viongozi wanaojua nini maana ya soka, hapo Zanzibar itainuka na kutajika.

No comments: