Tuesday 1 March 2016

Arsenal imetumia £3million kumsajili mchezaji huyu.



Kwa upande wa mashabiki wengine watasema sio swala la msingi kwao kwasababu wao wanataka matokeo ya sasa hivi na sio baadae. Lakini wengine wanataona kwamba huu ni uwekezaji muhimu kwa future ya club yao.
Taarifa mpya ni kwamba Arsenal imemsajili mchezaji mwenye miaka 17 kutoka Nigeria anaitwa Kelechi Nwakali ambae alikua mchezaji bora kwenye michuano ya World Cup U17 ndani ya Chile.
Wakala wa mchezaji huyo amethibitisha habari hizi kwa kusema, “Ni kweli Kelechi amesign mkataba wa miaka 5 na Arsenal na sitaweza kusema ni kiasi gani kimelipwa lakini ni zaidi ya Pound milioni 2”
Wataalamu wa mambo kwenye biashara ya soka wameshapata kiasi kilicholipwa ambapo ni pound milion 3 na Kelechi amesema kwamba anaenda Arsenal kuwa bora zaidi ya sasa.

No comments: