Thursday 19 May 2016

BLACK SAILOR NA MIEMBENI ZASHINDWA KUTAMBIANA.

Timu ya Black sailors pamoja na Miembeni zimeshindwa kutambiana katika mchezo wa ligi kuu ya Zanzibar kanda ya Unguja uliovurumishwa ndani ya dimba la Amani mjini Unguja.


Katika mtanange huo kila timu ilikuwa inataka kuondoka na alama tatu muhimu ili ziweze kuwaweka katika hatua nzuri ya kutinga nne bora kwa upande wa Unguja ili waweze kucheza katika kinyang’anyiro cha kuweza kulinyakuwa kombe la ligi hiyo.

Timu hizo licha ya kucheza vyema lakini hadi mtanange huo unamalizika hakuna timu ambayo imeona lango la mwenzake na hivyo kufanya kugawana alama katika mtanange huo.

Black sailor sasa wameshacheza  mchezo 22,wakiwa na alama 34 na wanakamata nafasi ya sita 6, wakati na Miembeni pia wameshacheza michezo 22,wakikamata nafasi ya saba 7, na alama zao ni 31 katika msimamo wa ligi kuu ya Zanzibar kanda ya Unguja.

Mpaka sasa ukiachana na JKU ambayo ina nafasi kubwa ya kuingia nne bora kwa Unguja,lakini timu tatu nyengine bado ni ngumu kuzijua ambazo zitaungana na JKU katika kinyang’anyiro hicho kutokana na alama walizonazo na jinsi marokeo ya mechi zao yanavyokuwa.

Ukiangalia msimamo wa ligi kuu ya Zanzibar kanda ya unguja JKU wana alama 50, Mafunzo alama 39, Zimamoto 36, KMKM,KVZ na Black sailors wote wana alama 34,Miembeni alama 31, Kipanga wa alama 30, Kimbunga alama 26,Jang’ombe boys alama 25, Chuoni alama 24,Kijichi wana alama 18, Polisi alama 14 na Mtende wana alama 10.

Kutokana na msimamo huo hakuna timu ambayo utaihesabu moja kwa moja katika kuelekea hatua ya nne bora.

No comments: