Friday 20 May 2016

ASTON VILLA YANUNULIWA NA MCHINA



Klabu ya soka ya Aston villa ambayo imeteremka daraja msimu huu katika ligi kuu ya England,hatimaye imenunuliwa na tajiri wa kichina Tony Xia ambaye ni mfanya biashara aliyewekeza katika sekta ya Michezo,Utalii,kilimo na afya.

Xia ameinunua Aston Villa kwa gharama ya dola milioni tisini (90), amesema amekuwa ni shabiki mkubwa wa klabu hiyo kwa miaka mingi ingawaje hajafurahishwa na matokeo mabovu ya msimu huu amabayo yamepelekea timu hiyo kushuka daraja.

Aston villa imeshuka daraja baada ya kuwa timu ya mwisho katika msimamo nafasi ya ishirini ikiwa na alama kumi na saba .

bbc

No comments: