
Timu ya Mafunzo imezidi kujiweka katika nafasi nzuri na kujipa matumaini ya kuweza kulitetea taji lao baada ya kuwafunga Timu ya Kikosi cha Valantia Zanzibar KVZ mabao 2-1, katika mchezo wa ligi kuu ya Zanzibar kanda ya Unguja.
Mchezo huo uliosukumwa
ndani ya uwanja wa Amani mjini Unguja, KVZ
walikuwa ndio wa mwanzo kupata bao lililowekwa kimyani na mchezaji
Suleiman Hassan Kede katika dakika ya nane 8.

Mafunzo wakasawazisha
mnamo dakika ya 30, kupitia mchezaji Sadik Habib, na mnamo dakika ya 41 Sadik
akarudi tena nyavuni kwa kuipatia Mafunzo bao la pili, na mabao hayo yalidumu
hadi kumalizika kwa mtanange huo kwa Mafunzo kuondoka na alama tatu kwa ushindi
wa mabao 2-1.
Katika mchezo huo
Mafunzo walicheza vyema katika kipindi cha kwanza, lakini kipindi cha pili KVZ
walicheza vizuri kwa kuutawala mchezo lakini walimaliza bila ya mafanikio
yoyote kwa kushindwa kuingiza bao katika kipindi hicho cha pili.
Baada ya mchezo huo
Mafunzo wamefikisha alama 32 wakiwa nafasi ya nne 4, na KVZ wapo nafasi ya pili
na alama 33.
No comments:
Post a Comment