
Nyota wa Cameroon Samuel Eto’o akimbizana na Mario Gomez kwenye kinyang’anyiro cha mfungaji bora.
Mshambuliaji wa
Cameroon Samuel Eto’o anayechezea kilabu ya Antalyaspor nchini Uturuki,
anaendelea kujijengea sifa kwenye ligi kuu ya soka ya Super Lig Spor Toto.
Eto’o ameonyesha
umahiri wake kwa kufungia Antalyaspor
jumla ya magoli 20 kwenye ligi katika mechi 31 zilizochezwa.
Kufuatia mafanikio
hayo, Eto’o anaendelea kukimbizana na mshambuliaji wa Ujerumani Mario Gomez
anayechezea kilabu ya Beşiktaş na ambaye kwa sasa amefunga jumla ya magoli 24.
Msemaji wa kilabu ya
Antalyaspor Hasan Ali Ceylan alibainisha umuhimu wa Samuel Eto’o kwenye timu
hiyo na mchango wake mkubwa alioleta katika mafanikio yao.
Vile vile, Ceylan pia
alifahamisha kwamba mchezaji huyo atapokea malipo ya ziada kufuatia makubaliano
yao ya mkataba kwa kuifungia magoli 20.
No comments:
Post a Comment