Monday 13 June 2016

Andy Murray arejea kwa Ivan Lendl

Mchezaji Tenisi Andy Murray hatimaye anaungana tena na kocha wake wa zamani Ivan Lendl kabla ya michuano ya Aegon .
Murray mwenye miaka 29, amekuwa bila kocha huyo muda mfupi kabla ya kuanza kwa michuano ya wazi ya ufaransa mwezi uliopita.
Mskoti huyo akiwa na kocha Ivan Lendl alishinda michuano ya wazi ya Wimbledon na Michuano ya wazi ya Marekani ya Olimpiki katika kipindi cha miaka miwili 2012-2014.
Lendl ni mshindi namba moja duniani na mshindi wa wa mara nane wa Grand Slam na amekuwa mtumishi katika chama au shirikisho la Tenisi la Marekani.

No comments: