Sunday 5 June 2016

Usain Bolt matatani baada ya mwanariadha mwenzake kufanyiwa ukaguzi



Mwanariadha Nesta Carter wa timu ya Jamaica ya mbio za kupokezana vijiti inayomjumuisha Usain Bolt anadaiwa kutumia dawa za kusisimua misuli baada ya kufanyiwa ukaguzi.

Nesta ambaye alishinda medali ya dhahabu pamoja na Bolt kwenye mashindano ya mbio za 4x100m za kupokezana vijiti kwenye olimpiki ya Beijing mwaka 2008 alifanyiwa ukaguzi na kugundulika kutumia dawa za kusisimua misuli.

Endapo Nesta atathibitishwa kutumia dawa za kusisimua misuli kwenye ukaguzi wa mwisho utakaofanyika, basi atawaweka wenzake matatani.


Hatua hiyo huenda ikasababisha Bolt kuvuliwa medali ya dhahabu moja aliyoshinda kwenye mbio hizo za 4x100m.

No comments: