Wednesday 9 March 2016

Mashabiki wa Real Madrid wamzoea Cristiano Ronaldo.

Licha ya kufunga goli ambalo limesaidia kwenye ushindi wa Real Madrid Vs Roma kwenye UCL, mashabiki wa Real Madrid wamemzomea mchezaji wao muhimu Cristiano Ronaldo..
Baada ya kitendo hicho kutokea Sergio Ramos moja kwa moja alikua upande wa Ronaldo na kusema kwamba, “Ningependa kuwaambia mashabiki kufikiria kidogo,ninawaheshimu sana lakini vitu visipoenda vizuri inabidi muda wote wawe upande wa wachezaji wao. Mafanikio kwa club ndio kitu ambacho wachezaji wote tunataka. Ronaldo ni mchezaji wa ki historia kwenye kikosi cha Real Madrid, anaendelea kuonyesha ubora kila mwaka”
Ronaldo anasema kwamba alikua qouted vibaya alivyosema wachezaji wenzake wangekua level kama yake basi wasingepoteza mechi dhidi ya Atletico Madrid. Kauli hiyo ndiyo imesababisha mashabiki kumzoea wakiitafsiri kwamba ni kudharau wenzake lakini yeye anasisitiza kwamba alimaanisha wengi walikua na injury lakini yeye hakuwa nayo.

No comments: