Katika mchezo huo mshambuliaji
Alexis Sanchez ndie alikuwa shujaa wa mchezo huo baada ya kuzipasia nyavu mara
mbili alianza kufunga goli la kwanza katika dakika ya sita 6, kisha akafunga goli la pili kwa mpira wa
adhabu katika dakika ya 38.
Katika mchezo huo timu
ya Arsenal iliutawala kwa asilimia 71, huku West Brom wao waliutawala kwa
asilimia 29.
Kwa ushindi huo vijana wa Profesa Arsenal
Wenger, wanajiweka katika nafasi nzuri ya kuwa kwenye nne bora baada ya
kujikusanyia alama 63 katika michezo 34 waliyocheza.
Arsenal wamesaliwa na
michezo minne mkononi kabla ya kumalizika kwa ligi kuu England msimu huu.
No comments:
Post a Comment