Mchezaji huyo mwenye umri
wa miaka 29 alimkaripia mwamuzi Jon Moss baada ya kufukuzwa uwanjani wakati wa
mechi ya Jumapili ambayo walitoka sare 2-2 na West Ham.
Kwa kukubali shtaka
hilo la Shirikisho la Soka la Uingereza (FA), Vardy, ambaye alikuwa ameitisha
kikao cha kujitetea, huenda akaongezewa adhabu juu ya adhabu ya sasa ya kutoruhusiwa
kucheza mchezo mmoja.
Klabu ya Leicester pia
imekiri shtaka la kukosa kudhibiti wachezaji wake wakati wa mechi hiyo.
Vardy, anayeongoza kwa
ufungaji mabao ligini, akiwa na mabao 22, atakosa mechi yao ya Jumapili dhidi
ya Swansea na akiongezewa adhabu huenda basi akakosa mechi dhidi ya Manchester
United tarehe 1 Mei.
Leicester, wapo alama
tano mbele ya Tottenham, na wanahitaji alama nane kutoka kwa mechi zao nne
zilizosalia ili kutwaa taji.
Mechi zao nne za mwisho
ni dhidi ya Swansea (nyumbani), Manchester United (ugenini), Everton (nyumbani)
na Chelsea (ugenini).
No comments:
Post a Comment