Sunday 12 June 2016

Manji, Sanga wapeta uchaguzi Yanga


Dar es Salaam. Matokeo ya awali yanaonyesha kuwa Mwenyekiti wa Yanga anayetetea nafasi yake, Yusuph Manji anaongoza kwa kura 1,468, na hakuna zilizomkataa, huku mbili zikiharibika.

 Akizungumzia uchaguzi huo ambao kura zimeendelea kuhesabiwa hadi asubuhi ya leo, Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano cha klabu hiyo, Jerry Muro amesema Clemence Sanga anaongoza katika nafasi ya Makamu mwenyekiti kwa kujikusanyia kura 1,428 dhidi ya mpinzani wake, Tito Osoro aliyekuwa amepata kura 80.

Hadi taarifa hizi zinapatikana kutoka Ukumbi wa Diamond Jubilee, jijini Dar es Salaam, klabu hiyo ilikuwa inaendelea na mchakato wa kuhesabu kura za wajumbe.Hata hivyo, Muro amesema matokeo kamili yatatolewa leo.

No comments: