Sunday 12 June 2016

Switzerland yailaza Albania

Switzerland imejipatia ushindi wake wa pili katika michuano ya bara Ulaya baada ya kuilaza Albania 1-0.
Mapema Albania ilionekana kubabaika pale mlinda lango wao Etrit Berisha alipofanya makosa kufuatia Krosi iliopigwa na Xherdan Shaqiri na hivyobasi kuwa rahisi kwa Schar kufunga kwa kichwa.
Lakini baadaye Armando Sadiku alikosa nafasi ya wazi kabla ya nahodha wa kikosi hicho Lorik Cana kupewa kadi ya manjano kwa kuunawa mpira.
Hatahivyo kushindwa kwa Switzerland kuongeza mabao kulifanya matokeo kusalia 1-0,lakini Shkelzen Gashi karibu asawazishe kwa upande wa Albania.
Mchezaji huo wa ziada alipata pasi nzuri huku ikiwa imesalia dakika tatu lakini Kipa Yann Sommer akaupangua mkwaju wake .

No comments: