Tuesday 8 March 2016

SOKA NA SIASA HAVYENDI PAMOJA

"KAMPENI YA FICHUA VIPAJI"



Wadau wa soka nchini wametakiwa kupunguza au kuondosha kabisa SIASA katika medani za soka ili kuruhusu vipaji vya wachezaji kukua.

Kauli hiyo imetolea leo na mchezaji wa Polisi  Mara daraja la kwanza Danny Manyenye wakati alipokua akizunguza na SALMA SPORT’S MEDIA  katika kampeni ya “FICHUA VIPAJI” ikiwa ni mchakato wa kuwatembelea, kuwakagua na kuwaonesha hadharani wachezaji wadogowadogo wenye malengo makubwa na mazuri katika soka.

Amesema viongozi wa soka nchini wamekua washabikiaji wa Siasa mpaka huiingiza katika soka hivyo hupelekea kukinzana baadhi ya mitazamo  baadae hutofautiana wao kwa wao hatime kutokua na maendeleo katika timu husika.

Sambamba na hayo pia Danny amesema Tanzania ina vipaji vingi sana mitaani lakini wanaotakiwa kuviendeleza hawaonekani na badala yake  wanasubiri kumuona anatoka chini mwenyewe kwa nguvu zake na anaposhindwa ndio humalizika kabisa kisoka.

Katika kutimiza ile kampeni ya “FICHUA VIPAJI” SALMA SPORT’S MEDIA imeshuhudia umahiri wa mchezaji huyu  mwenye jezi nambari 7 mgongoni na anaecheza nambari 9 na 10 uwezo wake wa hali ya juu unaonekana.

Sifa kuu iliyogundulika mara tu baada ya kuona uchezaji wake nikwamba ana mashuti mazito , pasi za mwisho pamoja na kupiga vichwa vya kiufundi.


Kutokana na changamoto zilizopo Danny amesema kama kweli nchi ina nia ya kua na wachezaji wazuri na taifa litajike hakunabudi kwa wadau wa soka na viongozi kutoa sapoti kwa timu za mpira,kuwaboreshea mazingira yao hapo nchi itakua tu kisoka.

No comments: