Sunday 29 May 2016

Real Madrid waibuka mabingwa.

Real Madrid wametwaa taji la ubingwa wa vilabu bingwa Ulaya kwa mara ya 11 baada ya kuichapa Atletico Madrid kwa mikwaju ya penati kwenye uwanja wa San Siro mjini Milan.
Bao la Sergio Ramos liliwaweka mbele vijana wa Zinedine Zidane kabla ya striker wa Atletico Antoine Griezmann hajakosa penati.
Mabadiliko yaliyofanywa na Diego Simeone kumuingiza Yannick Carrasco yaliupeleka mchezo huo extra time baada ya kuisawazishia timu yake kipindi cha pili.
Cristiano Ronaldo alipachika wavuni penati ya ushindi baada ya Juanfran kukosa penati yake kwa upande wa Atletico.
Kwenye hatua ya mikwaju ya penati, Lucas Vazquez, Marcelo na Gareth Bale walifunga kwa upande wa Real, wakati Griezmann, Gabi na Saul Niguezwakijibu mapigo na kufanya matokeo ya penati kuwa 3-3.
Baada ya Ramos kuifungia Real mkwaju wan ne wa penati, na kufanya matokeo kuwa 4-3, Juanfran wa Atletico akagonshwa mwamba penati yake iliyokuwa ya nne kwa upande wa Atletico na kutoa nafasi kwa Ronaldo kushinda taji.

No comments: