Timu ya Getafe imetangaza kumuondoa kocha wake Fran Escriba
kutokana na matokeo yasiyoridhisha kwenye ligi kuu ya soka ya La Liga nchini
Uhispania.
Katika mechi 12 za mwisho, Getafe imeweza kukusanya pointi 2
pekee kwa kutoa sare mechi mbili huku ikicharazwa mechi kumi.
Mara ya mwisho Getafe ilishindwa na Villareal 2-0 mwishoni
mwa juma lililopita na kuning'inia katika nafasi ya 19 kwa pointi 28.
Nafasi ya Escriba huenda ikachukuliwa na kocha Joaquin
Caparros ambaye aliwahi kufunza Sevilla, Athletic Bilbao, Mallorca na Granada.
No comments:
Post a Comment