Manchester City yatembeza kichapo kwa Cheslea
nyumbani
Timu ya Manchester City ilisafiri mjini London
kupambana na Chelsea kwenye mechi ya ligi kuu ya soka ya EPL nchini Uingereza.
Licha ya kucheza nyumbani, Chelsea ilishindwa kuleta
faraja mbele ya mashabiki wake na badala yake, wakapokea kichapo kikali cha 3-0
kutoka kwa Manchester City.
Mshambuliaji matata wa Manchester City Sergio Aguero
ndiye aliyefunga magoli yote matatu mojawapo likiwa ni kupitia mkwaju wa
penalti.
Kwa matokeo hayo, Manchester City wameweza kukusanya
jumla ya pointi 60 baada ya kucheza mechi 33.
No comments:
Post a Comment