Timu ya Manchester United ilisafiri ugenini kwenda kutoana
jasho na Tottenham Hotspur kwenye mechi yao ya ligi kuu ya EPL nchini
Uingereza.
Timu hizo mbili pinzani zilikabiliana vilivyo katika kipindi
cha kwanza na kuelekea mapumzikoni kwa sare ya 0-0.
Katika kipindi cha pili, wenyeji Tottenham Hotspur
walizidisha mashambulizi na kufanikiwa kuvunja ngome ya ulinzi ya Manchester
United.
Hatimaye Tottenham Hotspur ikafanikiwa kuitandika Manchester
United bao 3-0 na kuondoka na pointi 3.
No comments:
Post a Comment