Timu ya Liverpool iliikaribisha Stoke City nyumbani Anfield
kwenye mechi ya ligi kuu ya soka ya EPL nchini Uingereza.
Liverpool ambayo bado inajivuta kuwania nafasi ya kuingia 4
bora kwenye ligi ya EPL, ilikuwa sababu ya kutabasamu kwa kufanikiwa kuondoka
na pointi 3.
Wageni Stoke City walipokea kichapo cha Liverpool kwa
kucharazwa bao 4-1 kwenye mechi hiyo.
Kwingineko, viongozi wa ligi Leicester City nao waliendeleza
msururu wao wa ushindi baada ya kuwashinda Sunderland bao 2-0.
Ushindi huo umewawezesha Leicester City kuendelea kujikita
kileleni huku matumaini yao ya kushinda taji la EPL yakizidi kuongezeka.
No comments:
Post a Comment