Tuesday 10 May 2016

MICHEL PLATINI KUJIUZULU URAIS WA UEFA

Michel Platini kujiuzulu kama rais wa UEFA

Rais UEFA Michel Platini atangaza mpango wa kuachia ngazi kufuatia msimamo wa CAS

Rais wa UEFA Michel Platini ametangaza mpango wa kutaka kujiuzulu kufuatia uamuzi wa mahakama ya kimataifa ya soka CAS iliyompunguzia adhabu yake kutoka miaka 6 hadi 4.

Mawakili wa Platini walitoa maelezo na kuarifu mpango huo wa rais wa UEFA baada ya CAS kutoa uamuzi kuhusiana na adhabu yake.

Licha ya uamuzi wa CAS, Platini alisisitiza kuendeleza kesi hiyo kwenye mahakama za soka za Uswisi.

CAS iliamua kumpunguzia Platini adhabu ya kufungiwa kujihusisha na soka kutoka miaka 6 hadi 4 na faini ya fedha kutoka Franc 80,000 hadi 60,000.

Platini alitangaza kuweza kujiuzulu kutoka kwenye nafasi yake ya urais wa UEFA endapo mahakama ya CAS itakataa kufutilia mbali adhabu hiyo.

Rais wa zamani wa FIFA Sepp Blatter pia aliwahi kufungiwa miaka 8 na kutozwa faini ya fedha Franc milioni 2 kufuatia sakata la ufisadi lililokuwa likiwakabili.

No comments: