Sunday 13 March 2016

RASKAZONE NA NEGRO ZATOSHANA NGUVU KWA KUTOKA SULUHU YA BILA KUFUNGANA.


Timu ya Raskazone jana imetoka sare ya bila kufungana walipocheza na Negro katika mchezo wa ligi daraja la pili wilaya ya Mjini uliosukumwa ndani ya dimba la Amani.
Katika mtanange huo timu hizo zilionesha upinzani wa hali ya juu kwa kila timu kutaka kuondoka na ushindi, kwani zilipata nafasi nyingi za kufunga lakini umaliziaji ulikuwa ni mbovu kwa timu zote hizo.
Na mchezo huo ulimalizika kwa kutoka suluhu ya bila kufungana.
Akizungumza na SALMA SPORT MEDIA, kocha wa Raskazone Moh’d Shubeir (Babu shube) amesesma kuwa timu bado ni mpya na anahitaji kuitengeneza.
“Timu bado mpya natengeza na ina matatizo mengi unajua mpira tofauti na lai  kwenye friji asubuhi utaweka maji jioni utapata barafu huu mpira una mambo mengi, una mapungufu megi na ndio maana unachezwa katika sehemu ya wazi lakini bado najipanga kutengeza timu”.alisema kocha Shube.
Pia aliendelea kusema, “nilishasema na naendelea kusema nahitaji point tatu tu ili nibakishe timu katika daraja nimebakisha mechi tatu nahitaji point mbili inshaallah kwa uwezo wa mungu nitapata iyo nafasi na nitaibakisha hii timu mwakani nitatengeneza”.
Aidha  kocha wa timu ya Negro Hassan Abdul-Rahman Saidi amesema kuwa mechi ilikuwa ni nzuri,
“Mechi ilikuwa nzuri lakini nafasi tumezipoteza nyingi kiukweli ilikuwa si bahati yangu lakini nafasi tumezipoteza nyingi kwani wanapoingia katika maeneo ya umakini wanakuwa na presha na ndio wachezaji wetu wengi wa hapa Zanzibar,madhali nina muda wa kuiandaa timu vizuri hapa kwa sabau nimepewa siku kama nne saivi timu hii nategemea kwamba yatakuwa mambo mazuri kwa sababu nitafanyia mazoezi ya umaliziaji na muda mwingi tutafanya mazoezi ya umaliziaji”. Alisema kocha Hassan.

No comments: