Tuesday 22 March 2016

Tanzania kuikabiliana na Chad mengi yatarajiwa

Timu ya taifa ya Tanzania Taifa Stars itashuka dimbani hapo kesho, huko nchi Chad katika mchezo wa kuwania kufuzu kwa Fainali za Mataifa ya Afrika mwaka 2017.
Mchezo huo unatarajiwa kuchezwa majira ya saa 11 kwa saa za nyumbani Afrika Mashariki.
Taifa Stars, imefanya mazoezi ya mwisho kuelekea mchezo huo katika uwanja wa Omnisports Idriss Mahamat Ouya ulipo katika jiji la D'jamena.
Kocha anayekinoa kikosi hicho Charles Boniface Mkwasa amesema anashukuru vijana wake hakuna majeruhi na wote wameweza kufanya mazoezi aliyoyapangilia.

No comments: