Monday 21 March 2016

Van Gaal:Tuna fursa ya kutinga nne bora

Mkufunzi wa kilabu ya Manchester United Louis Van Gaal amesema kuwa harakati za timu yake kufuzu katika kombe la Vilabu bingwa Ulaya zingezimwa iwapo timu hiyo ingeshindwa na kilabu ya Manchester City,lakini sasa anaamini wana fursa kubwa ya kuwa katika timu nne bora.
Bao la Marcus Rashford liliipatia ushindi Manchester United dhidi ya wapinzani wao wa jadi Manchester City siku ya jumapili.
Kikosi hicho cha Van Gaal sasa kiko nafasi ya sita lakini kiko pointi moja pekee nyuma ya Manchester City walio katika nafasi ya nne.
''Pengo lililopo lingeongezeka iwapo tungepata droo ama hata kupoteza,ingekuwa vigumu sana'',alisema mkufunzi huyo wa United.Sasa hatma yetu iko mikononi mwetu lakini lazima tuendelee kushinda''.
''Tuna mechi nyingi za nyumbani ukilinganisha na zile za ugenini na hatushindwi sana katika uwanja wa Old Trafford,kwa hivyo tuna fursa''.

No comments: