Timu ya Yanga ya Dar-es Salaam ambayo imewasili visiwani
Pemba hapo jana kwa kuweka kambi ya kujiandaa na mchezo wa ligi kuu ya Tanzania
Bara dhidi ya timu ya Azam FC siku ya Jumamosi leo tayari imeanza kufanya
mazoezi kisiwani humo.
Yanga ambayo wakati wa asubuhi ilafanya mazoezi yake katika
fukwe za bahari zilizopo katika hoteli waliyofikia ya Pemba Misali Sunset
iliyopo Wesha nje ya kidogo ya mji wa Chake Chake lakini pia walilazimika kufanya
mazoezi wakati wa saa nane za mchana kijua kikiwaka uwanja wa Gombani kutokana
na jioni kuwepo kwa mchezo wa ligi daraja la kwanza taifa Pemba kati ya Masota
Rangers na Cossovo ya Wambaa.
Hata hivyo mazoezi hayo ambayo yakuhudhuriwa na mashabiki wengi
kama ilivyozoeleka kutokana na mashabiki hao kujongea katika uwanja wa Gombani
wakati wa saa kumi za jioni wakidhani kuwa Yanga watafanya mazoezi wakati huo.
Kwa mujibu wa taarifa ni kwamba kesho timu hiyo itafanya
mazoezi yake wakati wa asubuhi kwenye uwanja wa Gombani na saa 10 jioni kwenye
uwanja huo huo ambapo michezo ya ligi daraja la kwanza kisiwani humo sasa
itachezwa wakati wa saa nane za mchana.
Uongozi wa timu ya Yanga umesema kwa sasa hawatatoa taarifa zozote
juu ya mazoezi yao visiwani hapa hadi siku ya Ijumaa watakapozungumza na
waandishi wa habari baada ya kukamilisha kambi yao visiwani humo.
No comments:
Post a Comment