Thursday 14 April 2016

Barcelona yaaga ligi kuu ya kilabu bingwa ya UEFA



Atletico Madrid yaicharaza Barcelona na kufuzu nusu fainali ya ligi kuu ya UEFA.

 

Mabingwa watetezi Barcelona walifanya vyema katika mechi ya kwanza na kushindwa kuendeleza msururu wao wa ushindi kwenye mechi ya marudiano.

 

Atletico Madrid ilitembeza kichapo cha 2-0 kwa Barcelona na kuibandua kutoka kwenye kinyang'anyiro hicho cha kuwania kombe la ligi kuu ya UEFA.

 

Magoli yote mawili ya Atletico Madrid yalifungwa na mshambuliaji Antoine Griezmann katika dakika ya 36 na 88.

 

Baada ya matokeo hayo, sasa Atletico Madrid itasubiria mpinzani wake wa nusu fainali atakayebainishwa kwenye mchakato wa draw utakaofanyika siku ya Ijumaa.

No comments: