Miamba wa Uhispania Barcelona wamepokea kichapo cha tatu mfululizo La Liga baada ya kulazwa 2-1 na Valencia hapo jana.
Hii ni mara yao ya
kwanza kushindwa mechi tatu mfululizo ligini tangu 2003.
Kitulizo pekee kutoka
kwa mechi hiyo ni kwamba mshambuliaji wao matata Lionel Messi alifunga bao lake
la 500.
Ivan Rakitic aliingiza
wavuni krosi iliyotoka Guilherme Siqueira na kuwapatia Valencia uongozi wa
kushangaza.
Santi Mina baadaye
alifunga bao la pili dakika za mwisho za kipindi cha kwanza.
Barcelona sasa
wanaongoza ligi kwa kuwa wamefunga mabao mengi kushinda Atletico Madrid.
Barca wana alama 76 na
tofauti ya mabao 59 nao Atletico wana alama sawa lakini tofauti ya mabao 41.
Real Madrid wamo
nambari tatu na alama 75 na mabao 68. on goal difference.
Barcelona walikuwa alama
tisa mwanzoni mwa mwezi huu.
Barcelona, chini ya
mkufunzi wao Luis Enrique, walianza mwezi Aprili wakiwa alama tisa mbele ya
Atletico lakini uongozi huo umefutika upesi.
Walianza kwa kushindwa
na Real Madrid kwenye El Clasico.
Aidha, Atletico
waliwaondoa kwenye Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya wiki iliyopita.
Barca huenda
wakaondolewa kileleni iwapo watashindwa kupata ushindi ugenini Deportivo La
Coruna Jumatano.
Atletico watakuwa
ugenini Athletic Bilbao siku hiyo nao Real Madrid nyumbani dhidi ya Villarreal.
No comments:
Post a Comment