Vinara wa ligi kuu ya England walishindwa kuutumia vyema uwanja wao nyumbani wa King Power kwa kukubali sare ya mabao 2-2 na West Ham .
Jamie Vardy, aliipa
Timu yake uongozi kwa bao la kwanza katika dakika ya 18, mshambuliaji wa West Ham
Andy Carroll,akasawazisha bao hilo kwa mkwaju wa penati kabla ya Aaron
Cresswell kuongeza bao la pili kwa upande wa Wagonga nyundo.
Katika dakika ya lala
salama Jose Leonardo Ulloa akaisawazishia Leicester kwa goli la mkwaju wa
penati.
Matokeo hayo bado Leicester wanaendelea kushika uongozi wa ligi hiyo wakiwa na alama 73, wakati West Ham wao wapo nafasi
ya sita 6 na alama 53.
No comments:
Post a Comment