Ligi Kuu Tanzania bara
inaendelea tena leo kwa michezo mitatu kuchezwa katika viwanja mbalimbali
nchini.Huku kila timu ikisaka ushindi katika michezo hiyo ili kujiweka katika
mazingira mazuri kwenye msimamo wa ligi.
Young Africans watakua
wenyeji wa Mtibwa Sugar mchezo utaofanyika katika uwanja wa Taifa jijini Dar es
salaam.Ndanda FC wakiwakaribisha wakata miwa wa Kagera Sugar katika uwanja wa
Nang’wanda Sijaona mjini Mtwara.
Coastal Union
watawakaribisha maafande wa JKT Ruvu katika uwanja wa Mkwakwani jinini Tanga,
huku Jumapili, Simba SC wakicheza dhidi ya Toto Africans katika uwanja wa Taifa
jijini Dar es salaam
No comments:
Post a Comment