Murray asonga mbele robo fainali ya Monte Carlo Masters
Mchezaji wa tenisi
namba mbili duniani Andy Murray amefanikiwa kusonga mbele katika hatua ya robo
fainali ya Monte Carlo Masters baada ya kumfunga Benoit Paire.
Mwingereza huyo
ameshinda kwa seti 6-2, 7-5 7-5 katika muda wa saa mbili na dakika 33 dhidi ya
Mfaransa huyo.
Murray mwenye miaka 28,
sasa atakabiliana raia wa Canada Milos Raonic na Roger Federer huenda akachuana
na Rafael Nadal au Stan Warinka.
No comments:
Post a Comment